MAKAMU WA RAIS WA SMZ ATEMBELEA KITUO MAHIRI CHA KUTUNZA TAARIFA ZA KIMTANDAO -IDC



MAKAMU WA PILI WA RAIS WA SMZ ATEMBELEA KITUO MAHIRI CHA KUTUNZA TAARIFA ZA KIMTANDAO-IDC

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mh. Balozi Seif Ali Iddi akipata maelezo kutoka kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL Bw. Waziri Waziri Kindamba leo alipotembelea Kituo Mahiri cha Kutunza Taarifa za Kimtandao- IDC kinachoendeshwa na TTCL.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Mh. Balozi Seif Ali Iddi akipata maelezo kutoka kwa Afisa wa TTCL Bw. Deus Lwabukuna namna Kituo Mahiri cha Kutunza Taarifa za Kimtandao(IDC) kinavyofanya kazi.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akizungumza na wafanyakazi wa Wizara ya Mawasiliano, TTCL na wageni waalikwa baada ya kufanya ziara ya kikazi katika kituo hicho.Kushoto wa kwanza Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Miundombinu Selemani Kakoso, Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya TTCL, Mhe Omar Rashidi Nundu na Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Mohammed Khamis  Omari.

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Balozi Seif Ali Iddi akiwa katika kikao cha pamoja na wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano(sekta ya Mawasiliano), Bodi ya Wakurugenzi ya TTCL, Wafanyakazi wa TTCL na wageni kutoka Wizara mbalimbali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar, baada ya kukamilika kwa ziara  kutembelea IDC.
Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mhe. Balozi Seif Ali Iddi  akiwa katika picha ya pamoja na wafanyakazi wa Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano(sekta ya Mawasiliano), Bodi ya Wakurugenzi ya TTCL, Wafanyakazi wa TTCL na wageni kutoka Wizara mbalimbali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar, baada ya kukamilika kwa ziara  kutembelea IDC.

1 comment:

  1. kwa mahitaji passport size,green card ,passport za kusafiria usisite kupitia visafoto.com

    ReplyDelete